Wednesday, June 24, 2015

HOFU YA KUREJEA TENA KWA EBOLA FREETOWN YAZUKA

Ebola yaibuka mjini Freetown

Maofisa wa afya nchini Sierra Leone wamesema kwamba kuna wagonjwa wawili wapya wanaougua ugonjwa wa ebola na kwamba wamegunduliwa katika mji mkuu wa nchi hiyo Freetown.
Hapo awali ilidhaniwa kwamba mji huo ulikuwa hauna maambukizi ya ugonjwa huo,na hakukuwa na wagonjwa walioripotiwa hapo kabla kwa muda wa wiki kadhaa.
Naye msemaji wa kituo cha karantini cha taifa hilo amesema kwamba kulikuwa na wasiwasi mkubwa kwa sababu vituo vyote vya karantini  vitAendea kazi yake baada ya kufungwa mjini Freetown.
Kuna shaka kuwa kutatokea maambukizi mapya kutoka katika eneo lenye msongamano wa makazi duni.
Nako upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo ya Sierra Leone unaendelea kupata maambukizi mapya ya ugonjwa.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment