Monday, June 29, 2015

RHIHANA NA MIPANGO YAKE YA KUACHANA NA MUZIKI

Rihanna kaongelea kuhusu mipango yake, kagusia ukweli kuhusu kuacha muziki!

Celebrities watch the Los Angeles Lakers play the Los Angeles Clippers at the Staples Center. Clippers won by a score of 109 - 95 Featuring: Rihanna Where: Los Angeles, California, United States When: 07 Apr 2013 Credit: WENN.com
Robyn Rihanna Fenty maarufu kama Rihana ni mwimbaji, mtunzi wa nyimbo na fashion designer anaejulikana duniani kwa nyimbo nyingi kali kama Diamonds, Four Five Seconds aliomshirikisha Kanye West na Bitch better have my money, akiwa na miaka 27 tu Rihanna alishawahi kutajwa kama msanii mwenye ushawishi mkubwa duniani na pia kwa kipindi alichokuepo katika muziki ameweza kuweka ramani ya jina lake katika entertainment industry na kukubalika na mashabiki wa kila aina duniani.
Wiki hii headlines zinazomhusu Rihanna ni kuhusiana na yeye kuchukua time off kidogo kwenye muziki ili aweke nguvu na akili yake kwenye biashara ya mitindo kwa kuanza na line ya accessories itakayo kuwa inauza vitu mbali mbali kama hereni, mikufu, pete na vitu vengine kama hivyo.
Mwezi uliyopita, Rihanna kupitia kampuni yake ya Roraj Trade LLC alisajili baadhi ya hati miliki ya bidhaa zake ikiwemo brand yake mpya $CHOOL KIlls, jina lilosajiliwa na kupwea hati miliki pamoja na alama ya biashara tarehe 11 May mwka huu jijini New York chini ya kipengele cha Nguo na bidhaa za ngozi (Leather products and Clothing products). Brand hii mpya itakua inatengeneza vitu vingi baadhi vikiwa mapochi na badaae nguo.
Rihanna amesema bado anapenda muziki na hii haimanishi ana acha kabisa kufanya biashara ya muziki ila kwa kipindi hiki atakua amejikita zaidi kwenye biashara hii ya mitindo na sio muziki, ataendelea kutoa singles na albums ila sio kwa ukasi tuliouzoea kwani anapenda pia kuwekeza kwenye vitu vingine vya kumuingizia kipato hasa wakati huu ambao jina lake limekua kubwa ndani ya nchi na kimataifa na anahitaji kujitangaza kwa namna tofauti kwenye biashara tofauti anazopenda kuzifanya.
Kwa habari, taarifa matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment