Monday, June 22, 2015

JE, WAJUA UWANJA WA TAIFA MECHI NGAPI ZIMECHEZWA, MAJIBU HAYA HAPA

Ninayo majibu toka Bungeni kuhusu idadi ya mechi zote zilizochezwa Uwanja wa Taifa Dar…

U- Taifa Dar
Swali liliulizwa na Mbunge Victor Mwambalaswa Bungeni Dodoma leo June 22 2015 kuhusu idadi ya mechi zilizochezwa ndani ya Uwanja wa Kimataifa wa Mpira wa miguu uliopo Dar.
Majibu yakatolewa na Waziri Fenella Mukangala >>> “Mpaka sasa mechi 48 za Kitaifa na mechi 29 za Kimataifa zimechezwa katika Uwanja wa Taifa… Mapato yanayopatikana yanaelekezwa kwenye mfuko wa hazina wa Taifa. Mapato hayo hutumiwa na Serikali kama yalivyo mapato mengine
Kuna mpango wa kujenga Shule ya Michezo? >>> “Serikali haina mpango wa kuanzisha Shule ya Michezo kutokana na ufinyu wa Bajeti. Hata hivyo jitihada zinafanyika kuimarisha michezo katika Shule zilizopo” >>> Fenella Mukangala.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment