Wednesday, June 24, 2015

MPIRA MPYA UTAKAOTUMIKA LIGI KUU ENGLAND HUU HAPA

Cheki Mpira utakaotumiwa kwenye ligi ya England msimu ujao.

darren randolph new epl ball

Kukiwa kumesalia mizi miwili na siku kadhaa kabla ya ligi kuu ya England na lingi nyingine kubwa barani ulaya kuanza mpira rasmi utakaotumika kwenye ligi ya England umefahamika .
Mpira huo umebuniwa na kampuni ya vifaa vya michezo ya Kimarekani ya Nike ambapo utakuwa unafahamika kwa jina la Nike Ordem na umetengenezwa kwa kuzingatia teknolojia ya kisasa ambayo inaendana na mabadiliko ya mchezo wa soka .
Mpira huo umetengenezwa kwa kuzingatia jinsi ambavyo wachezaji watakuwa wakiutumia uwanjani ambapo moja ya vitu vilivyozingatiwa ni rangi yake na umetengenezwa kwa rangi ya ngavu ili kuwasaidia wachezaji kuuona wakiwa uwanjani na kufanya maamuzi ya haraka.
Beki wa West Ham United  James Tomkins akiwa anaujaribu mpira mpya ambao utatumika kwenye msimu ujao wa ligi ya England .
Beki wa West Ham United James Tomkins akiwa anaujaribu mpira mpya ambao utatumika kwenye msimu ujao wa ligi ya England .
Mpira huo pia una sehemu 12 ambazo zinaufunika ili kuusaidia kwenda na kasi ambayo itawasaidia wachezaji wenye uwezo wa kupiga mashuti ya mbali .
Mpira huo ambao unatarajiwa kuzinduliwa mwezi julai pia utatumika kwenye ligi za Hispania na Italia na umeonekana ukifanyiwa majaribio na wachezaji wa klabu ya West Ham United kwenye uwanja wao wa mazoezi .
Winga wa West Ham Matt Jarvis akionekana akijaribu mpira huu ambao pia utatumika kwenye ligi za Hispania na Italia .
Winga wa West Ham Matt Jarvis akionekana akijaribu mpira huu ambao pia utatumika kwenye ligi za Hispania na Italia .
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment