Wednesday, June 24, 2015

SOMA MAKUBWA YALIYOJIRI MAGAZETINI LEO, JUNE 24 TZ

Uchambuzi huu wa magazeti  unaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya kituo cha Elimu Cha Candle Education Centre Tanga. Kituo kinaongoza kufaulisha wanafunzi kidato cha pili hadi cha sita na wanaojiendeleza kielimu. Kituo kiko na huduma ya Hostel pamoja na kutoa kozi ya Kiingereza na Computer. Wapo Tanga mkabala na Bank ya CRDB simu 0715 7727246


s
logoMTANZANIA
Tume ya Taifa ya uchaguzi NEC, imesema haina mpango wa kurudia  uandikishaji wapigakura katika maeneo waliyopita kwani inaamini kazi hiyo imefanywa kwa ufanisi wa hali ya juu.
Pamoja na hali hiyo NEC imewaonya wanasiasa kutoingilia kazi yao kwa sababu wanaifanya kwa mujibu wa sharia za nchi, na hawapo kwa ajili ya kumwonea mtu bali kuandikisha na kusimamia haki za wapigakura.
Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya Waziri wan chi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenister Muhagama kusema kuwa NEC itafanya uchunguzi kubaini kama kuna ameneo ambayo wengi wameachwa bila kuandikishwa katika daftari la kudumu la wapigakura iliufanyike utaratibu wa kuandikisha.
Mwenyekiti wa NEC Damian Lubuva alisema hata kama hali hiyo itajitokeza, watarfikiria namna ya kurudia kazi hiyo, endapo utatolewa ushahidi wa wazi hasa kwa watu ambao hawakupata bahati.
“Siku ya mwisho kama kulikuwa na watu waliosalia ambao hawakuandikishwa kwenye vituo ambao hawakuandikishwa na waliorodheshwa na wanajulikana, tutafikiria, ikiwemo kurudia pale ambapo kutakuwa na ushahidi wa jambo hilo” Lubuva.
Alisema si wajibu wa NEC kwenda kutafuta watu eneo tofauti na lile lililopangwa kwa sababu hupangwa mapema mno baada ya kutolewa matangazo.
MTANZANIA
Wauguzi wa Zahanati ya Serikali katika kijiji cha Shishuyi Wilaya ya Maswa, wanadaiwa kumfukuza mjamzito Rotha Bujiku aliyefika katika Zahanati hiyo kwa ajili ya kujifungua na hatimaye kujifungua kwa taabu katika bafu la mkazi mmoja kijijini hapo karibu na Zahanati hiyo.
Watu walioshuhudia tukio hilo walisema lilitokea majira ya saa 2 asubuhi wakato Rotha alipofika katika Zahanati hiyo na kumkuta muuguzi Costansia John ambaye alikataa kumpokea.
Muuguzi huyo alikwisha  kupewa maelekezo tangu awali kuwa anatakiwa ajifungulie katika hospitali ya Wilaya ya Maswa kwa kuwa amekuwa akizaa watoto mfululizo.
Wakati mama huyo akiendelea kulalamika kutokana na uchungu aliokuwa akiupata, muuguzi huyo alimpigia simu Muuguzi Mkunga wa zahanati hiyo na alipofika alimweleza mjamzito kuondoka eneo hilo.
Rotha alilazimika kuondoa katika eneo hilo kusogea jirani na Zahanati hiyo na kujifungulia bafuni.
MWANANCHI
Boniface Mkwasa anakuwa kocha ghali zaidi Mtanzania baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutangaza kumlipa Dola 12,500 (Sh28 milioni) kwa kukubali kuchukua jukumu la kuinoa Taifa Stars.
Hiyo ni baada ya TFF kuamua kumpa kocha huyo msaidizi wa Yanga, mahitaji yote pamoja na mshahara aliokuwa akipokea kocha Mart Nooij, aliyetimuliwa Jumapili iliyopita baada ya kipigo cha mabao 3-0 kutoka kwa Uganda Cranes katika mchezo wa kusaka kufuzu kwa Chan 2016.
Rais wa TFF, Jamal Malinzi alisema kuwa Kamati ya Utendaji ya shirikisho hilo imekubaliana kwa pamoja kuwa Mkwasa apate stahiki sawa na zile za Nooij kama kielelezo cha kuonyesha jinsi ambavyo utawala wake unavyothamini makocha wazawa.
“Nilikutana na Mkwasa na kumwambia kuwa kile ambacho kocha aliyepita (Nooij) alikuwa anapewa, tutahakikisha naye anapata, kuanzia gari, posho nyumba na mshahara.
“Kwa kuwa suala la mshahara na nyumba ni jukumu la Serikali, tayari tumeshaiandikia barua kuwaambia kuwa tumeshapata kocha wa muda na tunaomba apate mahitaji yote ambayo aliyemtangulia aliyapata,” alisema Malinzi. w
Katika hatua nyingine, Malinzi amewashukia wachezaji wa Taifa Stars pamoja na baadhi ya makocha kuwa wamechangia kwa namna moja au nyingine kufanya vibaya kwa Stars kwenye michuano mbalimbali inayoshiriki.
“Kama Shirikisho tunapambana katika mazingira haya magumu tuliyonayo kwani wachezaji wetu ni hawa hawa na hatuwezi kuchukua kutoka nje ya nchi.
“Sasa, watu wanamwangushia lawama Malinzi kama vile yeye ndiye anatakiwa kucheza wakati hiyo ni kazi yao wachezaji.
“Hapa Tanzania kuna makocha kama 20 ambao wana leseni Daraja A, Nawapeni kazi ya kufanya utafiti halafu waone kati ya hao ni wangapi ambao wanafundisha, nadhani idadi yao haitazidi watano, wengine wamefungia ndani leseni zao, sasa kwa hali kama hiyo soka letu linaweza kupiga hatua,” alilalamika Malinzi.
MWANANCHI
Mbunge wa Geita (CCM), Donald Max (58) amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.
Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema kuwa mbunge huyo (pichani) alifariki jana saa 12.00 jioni katika hospitali hiyo.
Ndugai alisema Max alikuwa mahututi kwa kipindi cha takribani miaka miwili iliyopita.
“Taratibu za maandalizi ya mazishi kwa sasa bado maana ni kama dakika 15 zilizopita ndiyo kafariki,” alisema Ndugai.
Max alizaliwa Mei 22 mwaka 1957 na kusoma katika Shule ya Msingi ya Salvatorian Convent na baadaye kujiunga na Shule ya Sekondari ya Azania mwaka 1971 hadi mwaka 1974.
Mwaka 1980 alikwenda nchini Urusi na kusoma kozi ya ufundi katika Chuo cha Ufundi cha Roston on Don kabla ya kujiunga na Taasisi ya Volgograd Polytechnical nchini humo na kutunukiwa Shahada ya Uzamili katika Uhandisi.
MWANANCHI
Polisi mjini hapa wameyasambaratisha maandamano ya watu wasiofahamika waliokuwa na mabango ya kutaka muda wa uandikishwaji wa wapigakura kuongezwa.
Watu hao, ambao polisi iliwaita ‘wahuni’, waliandamana saa tatu asubuhi kwenye Barabara ya Sokoine.
Haikuweza kufahamika mara moja watu hao walitoka wapi, kwani wenyeviti wa mitaa ya kata zote hawakuweza kuwatambua.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema walilazimika kutumia nguvu kuvunja maandamano hayo kwa vile hayakuwa halali.
Sabas alisema watu hao ni kundi la wahuni lililozuka kutaka kusitishwa uandikishaji wa wapigakura.
Diwani wa Kata ya Sombetini, Ally Bananga alisema hakuwa na taarifa na maandamano hayo, lakini hashangai kutokea kwake.
“Sitashangaa watu kuandamana, kwani wamechoshwa na tabia ya watendaji kuwarudisha nyumbani. Watu wanafika asubuhi kituoni wanaambiwa warudi nyumbani kwa sababu hawakuandikisha majina yao,” alisema Bananga.
Mwenyekiti wa Mtaa wa JR, Jackson Mollel aliitaka tume kutoa mwongozo wa kuwasaidia wananchi kujiandikisha sehemu husika.
MWANANCHI
Mawaziri wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) na Wawakilishi kutoka CUF jana walitoka kwenye kikao cha bajeti cha Baraza la Wawakilishi, wakipinga urasimu katika utoaji vitambulisho vya ukazi wa Zanzibar na uandikishaji wapigakura.
Muda mfupi baada ya tukio hilo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) ilitoa taarifa yake ikisema kitendo cha mawaziri wa CUF kutoka kwenye kikao cha bajeti ni kuvunja katiba, kwa kuwa wameshindwa kuheshimu kiapo cha utii katika utekelezaji wa majukumu yao, kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1964.
Mawaziri hao walitoka nje ya kikao hicho muda mfupi baada ya Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano, Juma Duni Haji kusimama na kutoa malalamiko ya kutoridhishwa na utendaji wa SUK katika kusajili na kutoa vitambulisho hivyo vinavyotumika katika kuandikisha wananchi kwenye Daftari la Wapigakura.
Wakati wawakilishi hao wanaondoka ndani ya ukumbi, wenzao wa CCM walikuwa wakipiga makofi huku wakiimba “CCM, CCM, CCM”, na baadaye baraza kuendelea na muswada wa kupitisha mapato na matumizi ya bajeti ya mwaka 2015/2016.
Mawaziri waliohudhuria mkutano huo ni Abubakar Khamis Bakar ambaye ni Waziri wa Sheria na Katiba, Fatma Abdulhabib (Nchi, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais), Abdilahi Jihadi Hassan (Mifugo na Uvuvi) na Haji Mwadini Makame (Ardhi, Makazi, Maji na Nishati).
“Tumeamua kutoka ndani baada ya kuona wenzetu tuliowaamini, wametubadilikia. Hawana nia njema ya kuendesha serikali ya pamoja,” alisema makamu mwenyekiti wa CUF, Juma Duni Haji alipoongea na waandishi baada ya kutoka kwenye ukumbi huo.
“Wameanzisha Serikali ndani ya Serikali na sasa wanawanyima haki wananchi kinyume na katiba.”
Duni alisema kwa miaka mingi wananchi wamekuwa wakizungushwa kusajiliwa na kupewa vitambulisho vya ukazi, hali inayowaweka katika hatari ya kupoteza haki zao za kijamii, ikiwa ni pamoja na fursa ya kushiriki Uchaguzi Mkuu.
Hata hivyo, alisema uamuzi wao haujavunja katiba ya Zanzibar na kwa hiyo wataendelea na shughuli za Serikali kama kawaida.
Alidai kuwa kazi ya uandikishaji wapigakura kwenye Wilaya ya Magharibi, Unguja imetawaliwa na vitisho na kwamba watu wasiojulikana wamekuwa wakionekana wakiwa na silaha za moto na kujifunika vitambaa usoni mithili ya maninja na wengine kuvaa vinyago.
“Katika maisha yangu sijawahi kuona askari anayekwenda kulinda akificha uso na huu ni mkasa mpya duniani. Huwezi kumlinda raia kwa silaha za moto wakati yeye hana chochote zaidi ya mikono yake,” alisema Duni.
Naibu katibu mkuu wa CUF, Nassor Ahmed Mazrui alisema kuna vijana wamekwama kuandikishwa na kuitaka Serikali kuondoa urasimu katika upatikanaji wa vitambulisho vya ukazi.
NIPASHE
Serikali imesuuza roho za wastaafu nchini kwa kuwaongezea pensheni kutoka Sh. 50,000 wanayopata sasa hadi Sh. 100,000 kwa mwezi.
Hata hivyo, serikali imekataa kuondoa tozo la Sh. 100 kwa kila lita ya mafuta fedha zitakazoelekezwa katika miradi ya umeme vijijini (Rea) na miradi ya maji vijijini.
Katika Bajeti iliyosomwa Juni 11, mwaka huu, serikali ilipendekeza nyongeza ya pensheni kutoka Sh. 50,000 hadi Sh. 85,000 kwa mwezi.
Aidha, tozo ya mafuta ya dizeli na petroli kutoka Sh. 50 hadi 100 kwa lita na mafuta ya taa kutoka Sh. 50 hadi 150 kwa lita ili kuondoa uchakachuaji.
Waziri wa Fedha, Saada Mkuya, akijibu hoja mbalimbali za wabunge jana alisema jumla ya wabunge 98 walichangia mjadala moja kwa moja na wengine 13 kwa maandishi.
Alisema kwa kushirikiana na Kamati ya Bajeti, wametafakari michango ya wabunge 17 na kuona kiasi cha pensheni kilichoongezwa na serikali, bado hakitoshi na kwa kuzingatia kuwa ni wazee walioshiriki jitihada za kuleta maendeleo na kulifikisha taifa hapa lilipo.
“Serikali yenu imetafakari kwa makini, imekubali kuongeza ikiwa ni ongezeko la asilimia 100, tunatambua, tunathamini michango ya waliochangia taifa hili, tunatambua bado maisha ni magumu, lakini serikali yenu iko hapa itaendelea kufanya tathmini na mapato yakiridhisha, wataendelea kuongezwa,” alisema Waziri Mkuya na kuongeza:
Kuanzia Julai Mosi, mwaka huu, wastaafu wa kima cha chini watatoka Sh. 50,000 hadi Sh. 100,000…tutaimarisha mifumo yetu kuhakikisha wanaopunjwa, wanaokosa fedha zao, wananyanyaswa na watendaji, inakuwa thabiti pale alipo anapata pensheni yake.
Waziri huyo alisema wapo watendaji ambao wanashindwa kutoa majibu sahihi kwa wazee wanaofika Hazina na wanachukuliwa hatua na wataendelea kuchukuliwa kwa kuwa ni haki ya wazee na siyo upendeleo kwa kuwa wamechangia maendeleo ya taifa.
Alisema hoja ya mafao ya uzeeni ilichangiwa na wabunge 14, serikali imejipanga kuwatambua wazee kote nchini kwani kwa mujibu wa Takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, wapo milioni 1.2 na kwa sasa kuna ongezeko zaidi hadi mwaka huu kwani kuna waliofikisha umri na wengine wamefariki dunia.
“Kwa idadi hiyo tukisema tulipe kila mmoja Sh. 10,000 kila mwezi, tutahitaji zaidi ya Sh. bilioni 140, lakini hatujui makazi yao yalipo, hivyo kwa mwaka 2015/16, tunatoa fedha kwa maofisa wetu waende kuwatambua mahali walipo, tuwawekee mfumo ambao watapata fedha zao walipo,” alifafanua.
Alisema siyo wazee wote waliokuwa serikalini, lakini walichangia Pato la Taifa kwa shughuli zao kwenye sekta mbalimbali na kilio chao kimesikika na yote ni utekelezaji wa sera ya mafao kwa wastaafu.
Mkuya alisema serikali inafanya hivyo kwa kuwa kuna ripoti ya pensheni zinazopelekwa, lakini wahusika hawapati kutokana na mifumo na maofisa ambao siyo waaminifu wamekuwa wakishirikiana na benki kuchukua fedha  hizo.
NIPASHE
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk.Harrison Mwakyembe amesema kufungiwa kwa Tanzania kuuza mcheze katika soko la Afrika Mashariki linashughulikiwa na litapitiwa ufumbuzi ndani ya miezi miwili.
Kauli ya Mwakyembe imekuja siku chache baada ya Baraza la mchele Tanzania RCT kuiomba Serikali kushughulikia kufunguliwa kwa wafanyabiashara wa Tanzania wauze mchele katika soko la EA.
Mwakyembe alisema uamuzi wa kufungiwa kwa Tanzania naufahamu na  jambo hilo linashughulikiwa.
Alisema hatua alizoanza kuchukua ni pamoja na kukutana na Waziri wa viwanda na biashara wa Rwanda kujadili suala hilo.
“Tatizo lilikuwa kwa baadhi ya wafanyabiashara wasiokuwa waaminifu waliokuwa wakiingiza mchele kutoka nje na kuuchanganya na mchele wa ndani kasha kasha kuuza katika soko la Afrika Mashariki,”Mwakyembe.
Alisema nchi wanachama wa EA wana sharia ya kusameheana ushuru wa bidhaa zinazozalishwa katika nchi hizo pamoja na kodi ndogondogo.
HABARILEO
Serikali imekubaliana na umoja wa madereva katika madai yao waliyokuwa wakihitaji yatekelezwe, hali ambayo imemaliza tishio la kuwepo mgomo kwa mabasi yanayoenda mikoani pamoja na yale yanayofanya safari mijini.
Madai hayo ni pamoja na kupewa mikataba ya kudumu na waajiri wao, kukatiwa bima za afya pamoja kuongezewa mishahara.
Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa kikao kilichofikia makubaliano hayo, Katibu wa Umoja wa Madereva Nchini, Rashid Said alisema Serikali imekubali kusimamia na kutekeleza madai ya madereva ili kuepusha migomo ya mara kwa mara na kusababisha adha ya usafiri.
“Tumemaliza kikao chetu na mambo yote tuliyokuwa tunahitaji yatekelezwe yamekubalika. Lakini tumewaambia yatekelezwe ndani ya siku chache hizi na ifikapo Julai mosi mwaka huu kama hayajatekelezwa mgomo utakuwa pale pale,” Said.
Alisema wamefurahishwa na maamuzi ya kikao hicho ambayo yatakuwa ni mkombozi wa maisha ya madereva, kwani kwa muda mrefu wamekuwa hawanufaiki na kazi yao zaidi ya kuwazalishia wamiliki kiasi kikubwa cha utajiri, lakini wao kubaki katika hali duni ya maisha.
Hivi karibuni madereva walitishia kuanzisha mgomo endapo Serikali haitayashughulikia madai yao ambayo kwa muda mrefu wamekuwa wakipiga kelele yatekelezwe.
Mgomo wa madereva nchini ulitokea mwanzoni mwa Mei mwaka huu na kudumu kwa siku mbili na kusababisha kero mbalimbali kwa wasafiri huku asilimia kubwa ya wananchi wakitembea wakati wakienda katika shughuli zao mbalimbali huku waliokuwa wakienda mikoani kukwama katika kituo kikuu cha mabasi Ubungo.
Hata hivyo, mgomo huo ulisitishwa baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuunda Tume ya kushughulikia madai ya madereva ambayo hadi jana ilikuwa ikiendelea kujadiliana.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment