Thursday, June 25, 2015

TAARIFA TATA , BURUNDI BADO HAKUJATULIA

Makamu wa rais Burundi atoroka

Moja kati ya makamu wa rais wa Burundi ametoroka nchini humo baada ya kutangaza kuwa anapinga hatua ya rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu.
Makamu huyo  Gervais Rufikiri amekimbia Ubljiji  baada ya kuiambia runinga ya France24 kuwa muhula huo wa tatu unakiuka sheria na katiba ya taifa hilo.
Msemaji wa Serikali hata hivyo amekanusha madai hayo na kusema kuwa  Rufikiri amesafiri nje kwa ziara rasmi ya kikazi.
 Rufikiri amesema amekimbilia usalama wake akidai kuwa maisha yake yamo hatarini.
Msemaji huyo wa Serikali amesema iwapo  Rufikiri ametoroka Burundi ni kwa maslahi yake mwenyewe wala hakuna yeyote aliyemtishia maisha yake.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment