Tuesday, June 2, 2015

BASHRI KUAPISHWA BAADA YA KUSHINDA UCHAGUZI BILA KUWA NA MPINZANI

Rais Bashir aapishwa kwa muhula mwengine

Rais Omar al-Bashir, ameapishwa kwa muhula mwengine wa miaka mitano baada ya kupata ushindi mwengine kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika April.
Al- Bashir,angali na kesi Mahakama ya Kimataifa, The Haghe (ICC)  inayomtuhumu kwa mauaji yaliyofanywa dhidi ya baadhi ya wakaazi wa Darfur, nchini humo.
Uchaguzi huo  ilisusiwa na vyama vya upinzani lakini ikaendelea licha ya wapiga kura wachache kujitokeza..
Viongozi wa Kenya , Misri na Zimbabwe ni baadhi ya waliohudhuria sherehe hiyo ya kuapishwa kwa Al Bashir ambaye amekuwa madarakani tangu alipochukua hatamu za uongozi kupitia mapinduzi ya mwaka 1989.
Kwa habari na matukio ya papo hapo , ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment