Wednesday, June 3, 2015

RAFAEL NADAL HAVUMI LAKINI NAE YUMO

Bei ya saa ya staa wa Tennis Rafael Nadal nayo kwenye headlines..

nadaa
Ukiwazungumzia wanamichezo ambao wana utajiri mkubwa zaidi duniani jina la Cristiano Ronaldo, Floyd Mayweather au Messi huenda ndio wanaoongoza kwa kuwa na utajiri mkubwa zaidi.
Kuna wanamichezo wengine ambao ni nadra kuwasikia wakijitangaza au kutajwa kuwa na utajiri mkubwa lakini mmoja wao ni mcheza tenis Rafael Nadal ambaye naye ameamua kuonyesha jeuri ya fedha.
nadal2
Wakati wa michuano ya French Open alipokuwa akipambana na Jack Sock, Nadal alivaa saa yenye thamani ya pauni 510,000 ambazo ni sawa na fedha za kitanzania zaidi ya bilioni 1.7.
Saa hiyo aina ya  RM27-02 imetengenezwa na kampuni ya Luxury Swiss na unaambiwa kampuni hiyo ilitengeneza saa 50 tu za aina hiyo ambayo moja imevaliwa na mchezaji huyo.
huyu
Rafael Nadal ni bingwa wa michuano ya French Open mara tisa.
Kwa habari na michezo pamoja na matukio mbalimbali ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment