Tuesday, June 2, 2015

STEP BLATTER AJIUZULU

Rais wa FIFA Sepp Blatter kujiuzulu


Rais wa Shirikisho la Soka Duniani FIFA Sepp Blatter amesema kuwa atajiuzulu kama Rais wa Shirikisho hilo kufuatia kashfa ya ufisadi.
Akitangaza kujiuzulu,kwake Sepp Blatter mwenye umri wa miaka 79 ameitisha kikao cha dharura mara moja ili kumchagua rais mpya.
Blatter alichaguliwa tena wiki iliopita licha ya maafisa wake saba wakuu kukamatwa siku mbili kabla ya uchaguzi .
Lakini alisema kuwa mamlaka yake hayaungwi mkono na kila mtu.
Kwa habari na mtukio ya ukweli na uhakika usiache kuwa mbali nami, na niko tayari kukupatia kinachonifikia hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment