Wednesday, June 22, 2016

MAJI BARABARA YA 15 HAYANA PAKUPITA YAZALISHA MAZALIA YA MBU NA VYURA



Maji machafu yakiwa yametuwama hadi kubadilika rangi na kusababisha  mazalia ya mbu na kuwa kero kwa wakazi wa eneo hilo la barabara ya 15 Swahili Street. Ngamiani Kusini Tanga.
Mbali ya jitihada za halmashauri ya jiji kuisafisha inadaiwa kuwa baadhi ya kaya ni chanzo cha mifereji kuziba kwa kutupa takataka na kuiacha kuisafisha.
Wataalamu wa mazingira wameiambia tangakumekuchablog kuwa ni vyema sheria ndogondogo kufuatwa ili kuwezasha mji kuwa msafi na kuchukuliwa hatua kwa wanaokaidi kufanya usafi na kuweka mazingira katika maeneo yao na kuacha dhana ya kuwa Serikali ndio yenye jukumu la kuisafisha.






Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment