Sunday, June 19, 2016

IBADA YA KUAGWA MWILI WA JO COX KUFANYIKA LEO



 
 Ibada ya kumkumbuka mbunge wa Uingereza aliyepigwa risasi na kuuwawa juma lililopita Jo Cox, itaandaliwa leo Jumapili katika makanisa mawili huko Birstall - West Yorkshire.
Kitabu cha maombolezo pia kitafunguliwa kwa wale ambao wanataka kutoa rambirambi zao kwa mwanasiasa huyo aliyeuwawa siku ya Alhamisi alipokuwa akienda kwenye kituo cha upasuaji, katika eneo bunge lake.
Hapo jana familia ya mbunge huyo, ilifika mahala aliposhambuliwa na kuzingirwa na watu wa Birstall.
BBC

No comments:

Post a Comment