Friday, June 24, 2016

CAF YAITOA ES SETIF LIGI YA MABINGWA

CAF imetangaza kuitoa ES Setif Ligi ya Mabingwa Afrika

June 24 2016 shirikisho la soka barani Afrika CAF limetangaza maamuzi magumu ya kuitoa klabu ya ES Setif ya Algeria katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, katika hatua ya nane bora hivyo kufanya Kundi B libaki na timu za Enyimba, Mamelodi Sundowns na Zamalek.
CAF wamefikia maamuzi hayo baada ya kukaa chini na kupitia vifungu vya sheria, ni adhabu gani inastahili kwa klabu hiyo, ambayo imetolewa katika mashindano hayo kwa kosa la mashabiki wake kufanya fujo katika uwanja wao wakati wa mchezo dhidi ya Mamelod Sundowns ya Afrika Kusini June 19 2016.

No comments:

Post a Comment