Monday, June 20, 2016

KERO YA MAJI MKINGA SUGU



Tangakumekuchablog
Mkinga, WAKAZI wa kijiji cha Mwanyumba kata ya Bwiti  Tarafa ya Maramba Wilayani Mkinga Mkoani Tanga, wameitaka Serikali kurejesha mfumo wa upatikanaji wa maji safi baada ya miundombinu yake kuchakaa.
Wakizungumza na waandishi wa habari juzi, wakazi hao wamesema hali za afya zao ziko mashakani baada ya kutumia maji ya mto ambayo pia hutumiwa kwa ajili ya kunyweshea mifugo.
Walisema mbali ya uchakavu huo unapotokea ujio wa viongozi wa Serikali maji hutoka katika mabomba na kuwapa mashaka wa upatikanaji wa maji wa kila siku na kuondokana na kupatwa na magonjwa ya tumbo na kichocho.
“Ajabu hapa tuko na mwaka bomba halitoi maji lakini ujio wa viongozi wa Serikali imekuwa neema kwetu, tumekuwa tukitumia maji ya mito ambayo pia hutumiwa na wanyama” alisema Asha Bakary na kuongeza
“Usikiapo ujio wa viongozi wa kitaifa ujue  maji yatatoka ila tatizo hatuna vifaa vya kuhifadhia , ila leo ni sikukuu ya wa watu wa Mwanyumba” alisema
Alisema kuna kitisho cha kuzuka kwa magonjwa ya tumbo na kichocho baada ya wakazi wote kutumia maji ya mto kwa matumizi ya kunywa kupikia na kuongea wakiwemo wanyama.
Akizungumzia kero hiyo, Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji kata ya Magati, Kimwaga Shauri, alisema  uhaba huo wa maji kijiji cha Mwanyumba imetokana na vijiji kuongezaka ambapo awali kijiji hicho kilikuwa hakimo katika mradi wa maji.
Alisema kuongezaka kwa vijiji imekuwa sababu ya baadhi ya maeneo kukosa maji kwa baadhi wa wakati na kusema kuwa Serikali inafanya jitihada za kuhakikisha vijiji vyote vinafikiwa na maji safi na salama.
“Mradi wakati ulijengwa ulikuwa wa vijiji vitatu na  sasa tuko na vijiji saba jambo ambalo linatupa wakati mgumu kuyagawa na kuzifkia kaya ikiwemo kijiji cha Mwanyumba ambacho hakikuwemo katika mradi” alisema Shauri
Alisema jitihada za kuhakikisha maji yanapatikana kijijini kwa kutumia mfumo wa zamu unafanyika na kuwataka wananchi kulinda vyanzo vya maji na kuacha kukata miti .
                                                  Mwisho






Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment