Thursday, June 23, 2016

KOREA KASKAZINI YAFANIKIWA KURUSHWA KOMBORA LA MASAFA MAREFU

Korea Kaskazini yadai uwezo wa kulipua Marekani

Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, amesema kuwa taifa lake linauwezo wa kushambulia maeneo yote  ya Marekani, katika bahari ya Pacific.
Rais Kim Jong alisema hayo baada ya taifa lake kufanikiwa kutekeleza majaribio ya makombora yenye uwezo wa kusafiri mwendo wa kasi..
Wataalamu wa kijeshi wa Marekani na Korea Kusini wanasema kwamba kombora moja lilishindwa kulipuka ilihali la pili ilifaulu kwenda zaidi ya mamia ya kilomita.
Korea Kaskazini imesifia pakubwa uwezo wake huo wa kuunda silaha za kitonoradi.
Wanachama wa baraza la usalama la Umoja wa mataifa wamekutana na kuelezea kushtushwa  kwao na hatua hiyo ya Korea Kaskazini.
BBC

No comments:

Post a Comment