Sunday, November 30, 2014

Fuso lauwa watu 7 Korogwe



Kumekucha Blog

Korogwe, SIKU nne tangu itokee ajali mbaya iliyohusisha basi dogo la abiria  na lori Muheza Mkoani Tanga na  kuuwa watu 13 na wengine 25 kujeruhiwa jana gari la mizigo lilillojaza watu lilipoteza njia na kuuwa watu 7 na wengine 14 kujeruhiwa.

Ajali hiyo ilitokea saa 1 jioni kijiji cha Magundi kata ya Mbungu  watu waliokuwa wakitokea mnadani waliokuwa wamejazana katika gari aina ya Mistubishi Canter iliacha njia na kupinduka na kusababisha vifo vya watu 7 papo hapo.

Ajali hiyo iliyothibitishwa na kamanda wa polisi Mkoa wa Tanga, Fraisser Kashai na kuwataja watu waliofariki kuwani, Ali Juma (47), Kihiyo Rutha, Merina Kiteleko, Asha Mussa, Stella Chales(32)   Mama Kivula na Jane Mbajo na miili yote imehifadhiwa hospitali ya Wilaya ya Magunga.

Kamanda Kashai aliwataja waliojeruhiwa Este Akili, Amina Mohammed (23), Ramadhani Omar (32)Amina Rajab(32) Veronica Daniel (18), Mwaliki Pitter, Jarnet Chales(40), Mariama Sadick (45), Said Salinza (42) Mgoshi Bashiri (48) Monica Chales(40), Veronica Kiondo (43), Zaina Hamis(24) na  Richard Mosess.

Akieleza chanzo cha ajali hiyo kamanda Kashai alisema Polisi inamshikilia dereva wa gari hilo,  Ramadhani Omar kwa uvunjifu wa sheria za barabarani baada ya kuchukua abiria kinyume na sheria.

Alisema dereva huo alipatwa na tamaa ya kupata pesa baada ya kumaliza kasi yake ya kupeleka mazao masokoni na bidhaa katika minada hivyo kuchukua abiria kinyume na sheria.

Alisema watu hao ambao walikuwa wengi dereva huyo alishindwa kulimudu gari lake na wakati akikata kona ilimshinda na kuingia porini kisha kupinduka na watu saba kufa papo hapo.

“Tulitoa agizo kuwa magari ambayo hayaruhusiwi kubeba abiria kuacha kufanya hivyo---lakini agizo hili naona halitekelezwi na hivyo sasa ni kazi moja tu ya kufikishana mahakamani” alisema Kashai

Akitoa agizo kwa wananchi kamanda huyo amewataka kutoa taarifa kwa jeshi la polisi pale wanapoona sheria za barabarani zikikiukwa ikiwa na pamoja na mwendo kasi na upakiaji wa abiri kupindukia.
                                                                    Mwisho

No comments:

Post a Comment