Tuesday, November 25, 2014

Wajawazito Korogwe waaswa



Kumekucha Blog

Korogwe,WAKUNGA Wilayani Korogwe Mkoani Tanga, wameitaka jamii ya mama wajawazito kuwa na ada ya kuhudhuria vituo vya afya vipindi vya ujauzito na kukemea tabia ya baadhi ya watu kujifungulia sehemu zisizo tambulika.

Wakizungumza katika mafunzo kwa wakunga vituo vya afya Wilayani humo juzi,yaliyoandaliwa na Chama Cha Wakunga Tanzania (TAMA)  walisema wamekuwa wakipata wakati mgumu kumpokea mjazito ambaye hajawahi kuhudhuti kliniki.

Walisema kuna baadhi ya wajawazito wamekuwa wakisahau wajibu wao wa kuhudhuria kliniki wakati wa ujauzito na hivyo kipindi cha kujifungua hufika vituo vya afya na kuwa shida baada ya kutokuwa na kumbukumbu za ujauzito huo.

“Tuko na changamoto nyingi sisi wakunga hasa pale ambapo mama mjamzito anapofika siku ya kupata uchungu wa uzazi na hivyo kushindwa namna ya kumpokea” Chevu Mkufya

Alisema ili kujiepusha na matatizo wakati wa kujifungua amewataka mama wajawazito kuhakikisha wanapopata ujauzito tu kuanza kliniki na kudai kuwa hiyo itasaidia kupunguza vifo vya mtoto wakati wa kujifungua.

Kwa upande wake  Mratibu wa wafunzo hayo Martha Rimoi aliwataka watumishi hao kuwa mabalozi wazuri katika vituo vyao lengo likiwa ni kutokomeza vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua.

Alisema kufuatia kukithiri wimbi la wasichana kuzaa muda umri mdogo ni wajibu wa wakunga kutoa elimu mashuleni na kwa njia ya televisheni katika maeneo ya wazi ili kila mmoja kutambua wajibu wake.

“Ninyi wakunga ndio muonaojua kero ambazo munakabiliana nazo hebu jipangeni na hata kuomba bajeti ili kuandaa vipindi vya maonyesho vya televisheni jamii itambue ubaya na uzuri mjazito nini anatakiwa kufanya” alisema

“Mimba za utotoni zimekuwa zikiongezeka siku hadi siku hivyo ni vyema kuwa na utaratibu wa kutoa elimu mashuleni na katika viwanja vya wa wazi na kusaidia kutokomeza matatizo ya wazazi wakati wa kujifungua” alisema Rimoi

Alisema kufanya hivyo kutasaidia kuwafanya wazazi na wajawazito kutambua wajibu wao vipindi vya kubebea ujauzito na hivyo kuwataka kuwa na mikakati ya kulimaliza tatizo hilo kwa wajawazito.

                                                       Mwisho

No comments:

Post a Comment