Wednesday, November 26, 2014

Kutoka Bungeni



Novemba 26 Bungeni Tz, ishu ya Escrow na agizo la Mahakama kuzuia mjadala wa Ripoti ya CAG


investigation
Wakati Kikao cha Bunge kikiendelea Dodoma leo, miongozo bado iliendelea kuombwa na baadhi ya Wabunge kuhusiana na suala ambalo limechukua siku kadhaa sasa kwamba Mahakama ilitoa agizo la kuzuia Bunge kujadili kuhusiana na Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu Wa Serikali CAG, leo Novemba 26 Wabunge Suleiman Nchambi, Esther Bulaya, Tundu Lissu, Ole Sendeka na Joshua Nassari waliomba mwongozo kuhusiana na hilo.
Mbunge Nchambi alianza kwa kuuliza; “… Watanzania waelewe wazi sisi wabunge wa Chama cha Mapinduzi tunayo dhamira ya kujadili jambo hili Bungeni na kwa kuwa CHADEMA wameonyesha waziwazi kupitia mjumbe wao kuwa wanapinga suala hili, naomba mwongozo wako kwanini wakati tunajadili suala hili zito tusijadili pia suala hili zito la mjumbe wa CHADEMA kwenda kupinga kujadiliwa hoja hiyo hapa Bungeni…
Tundu Lissu akajibu hoja hiyo; “… Anaitwa Gabriel Mnyele, mkazi wa Mpanda ni mwana-CCM na wasiofahamu mimi nimesoma naye… Wakili wa Pan African Power Solutioms anafanya kazi kwenye kampuni moja ya uwakili na Mabere Marando, isipokuwa Wakili Mabere Marando hajahusika kwa namna yoyote ile na kesi iliyopelekwa Mahakamani...”
Kuusikiliza mjadala huo wa Bunge bonyeza play hapa.
Hakuna story itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote.

No comments:

Post a Comment