Wednesday, November 26, 2014

Soma ukatili huu wa wenza wamoja

Isome hii ya mke aliyeamua kushirikiana na mumewe kumbaka binti wa miaka17


pregna
Mwanamke mmoja nchini China ambaye ni mjamzito amehukumiwa kifungo cha maisha huku mume wake akihukumiwa adhabu ya kifo baada ya kushirikiana kumbaka na kisha kumuua msichana wa miaka17.
Mwanamke huyo ambaye anajulikana kwa jina la Tan Beibei alifanya kitendo hicho baada ya msichana huyo kumsaidia alipoanguka barabarani ambapo alimpeleka hadi nyumbani kwake na badala ya kumshukuru waliamua kumfanyia kitendo hicho cha akishirikiana na mumewe kisha kumuua na kuamua kumzika.
Mahakama ya Heillojiang ya nchini humo imesema kuwa imewafungulia mashtaka ya kuua,kubaka pamoja na kushambulia baada ya mwanamke huyo kujifanya ni mgonjwa na kushirikiana na mumewe kumfanyia binti huyo kitendo hicho cha kudhalilisha kisa wivu kwa madai alikua akitembea na mumewe.
Mahakama ya juu ilikataa kuwapunguzia adhabu wawili hao baada ya kukata rufaa kwa madai kesi hiyo ni kubwa na haina dhamana yoyote.
Kwa mujibu wa mashuhuda msichana huyo aliyejulikana kwa jina la Hu alikua akipita barabarani ndipo mama huyo alipomwomba msaada wa kumpeleka nyumbani kwake baada ya kuanguka na msichana huyo kutii lakini alipofika alikutana na maswaiba hayo.
Inaelezwa kuwa baada ya kufika mume wa mwanamke huyo alimpa msichana huyo maziwa ya mtindi na baadaye kuanza kumfanyia kitendo hicho akishirikiana na mkewe lakini hata hivyo hawakufanikiwa kwani binti huyo aliweza kuwazidi nguvu na walipoona imeshindikana walichukua blanketi na kumziba nalo usoni hadi alipofariki dunia na kuamua kumzika.
hands
Katika utetezi wa mwanamke huyo mahakamani hapo alisema aliamua kufanya kitendo hicho kwa sababu binti huyo alikua akitembea na mume wake.
Historia inaonyesha wawili hao walishawahi kuwa na kesi mbalimbali kiwemo ya kutaka kumbaka rafiki wa mtoto wao wa kike ambaye alikua akisoma naye darasa moja

No comments:

Post a Comment