Saturday, November 22, 2014

Leo habari kubwa magazetini


Leo Novemba 22 nimekuwekea hapa Story kubwa kwa undani zilizoandikwa Magazetini.

Leo Novemba 22 nimekuwekea hapa Story kubwa kwa undani zilizoandikwa Magazetini.

stock-footage-days-flying-logo-saturday
MWANANCHI

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro amepiga marufuku unywaji wa pombe kali aina ya Viroba kwa watu wenye umri kati ya miaka 18-30 pamoja na kupiga marufuku uuzaji wa pombe kiholela.

Waraka uliotolewa na Mkuu wa Mkoa huyo umeonyesha kuanzia Desemba 15 Serikali itaendesha oparesheni maalum ya kuwakamata  watu wanaolewa pombe muda wa kazi.

Akielezea hilo Mkuu huyo wa Mkoa amesema ulevi uliokithiri umepelekea kupungua kwa nguvu kazi ya kutosha kutokana na vijana wengi kujiingiza katika unywaji wa pombe unaoathiri afya zao.

MWANANCHI

Mtu mmoja amefariki kutokana na tetenasi ambayo ilisababishwa na kidonda alichokipata wakati anabandua kucha za bandia alizobandika wakati siku ya harusi yake.

Mtu huyo Sophia Komba alifunga ndoa Oktoba 15 na Richard Mmary, ambapo mume wake anasema wiki moja baada ya kufungwa ndoa hiyo Sophia alimuaga anaenda saluni  kutoa kucha, aliporudi baada ya saa mbili alikuwa analalamika sana kuumwa na kidole ambacho kilipata kidonda kutokana na kubanduliwa kucha vibaya na kuumia.

Mume wake anasema hakujua ukubwa wa tatizo hivyo akamnunulia Spirit na kumpaka, lakini tatizo likaendelea kuwa kubwa na mpaka anafariki daktari alithibitisha kuwa mwanamke huyo amefariki kwa tetenasi.

Wamiliki wa saluni waliohojiwa wamesema kuwa gundi inayofaa kubandikia kucha huuzwa ghali hivyo huenda saluni iliyomhudumia marehemu huyo walitumia gundi ya bei nafuu ambayo siyo salama, huku mtu mwingine anayejishughulisha na kubandika kucha hizo akisema iwapo kucha hizo zinakaa muda mrefu huwa na madhara kwa binadamu.

                                                Mwisho

No comments:

Post a Comment