Wednesday, June 3, 2015

KITISHO CHA NDOVU KUTOWEKA TZ YATANDA

Idadi kubwa ya ndovu yatoweka Tanzania


Wanaharakati wa wanyamapori wameelezea hali ya kutoweka kwa idadi ya ndovu kwa asilimia sitini nchini Tanzania katika kipindi cha miaka mitano iliyopita kama janga.
Kwa mujubu wa kikundi  kinachofuatilia maisha ya wanyamapori, TRAFFIC, linasema idadi hiyo inaashiria kiwango halisi cha uwindaji haramu.
Waziri wa Maliasili na Utalii   Tanzania Lazaro Nyalandu, amesema kuwa tatizo hilo lipo kwa kiwango tofauti nchini humo, akitoa mfano kuwa eneo la Serengeti idadi yao inaongezeka .
Amesema mamia ya walinzi wa wanyamapori wamekodiwa kukabiliana na uwindaji haramu

No comments:

Post a Comment