Monday, December 21, 2015

FABRIGAS AIBUKA NA KUSEMA HAYA

Baada ya Fabregas kuzomewa na mashabiki wa Chelsea, Pedro kaamua kuongea haya ….

December 19 Ligi Kuu Uingereza iliendelea na moja ya mechi zilizochezwa ni ile ya Chelsea dhidi ya Sunderland, mchezo uliomalizika kwa Chelsea kuibuka na ushindi wa goli 3-1. Katika mchezo huo, mashabiki wa Chelsea walionekana kumzomea Fabregas kwa kauli yake aliyoitoa juu ya Diego Costa kuwa anachangia kupata matokeo mabovu kwa timu hiyo.
fabregas-costa-chelsea-sunderland-banner-fans_3390270
Mshambuliaji Pedro Rodriguez hakufurahishwa na kitendo hicho hivyo kufikia hatua ya kumpa maneno yenye faraja kiungo Cesc Fabregas, baada ya kuzomewa na mashabiki wake kwenye mchezo na Sunderland wakati bado anaamini bado ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa.
Fabregas-Chelsea-547156
“Ulikuwa ni wakati mgumu kwake ila ninaamini anapitia wakati mgumu, ni mchezaji imara, mwenye uwezo mkubwa na ana sifa nzuri ndani ya klabu na ni mshindi mpaka hapo alipo. Ninaelewa mashabiki wetu wana hasira kwa sasa, na hii ni hali ya kawaida pindi timu na Kocha wanapokuwa katika hali kama hii” >>>>Pedro.
Kauli ya Cesc Fabregas ilikuja siku chache kabla ya uongozi wa klabu ya Chelsea haujamfukuza aliyekuwa kocha wa timu hiyo Jose Mourinho. Hivyo lawama za Fabregas kwa Diego Costa zimemfanya aingie katika matizoni kwa mashabiki kumzoea kutokana na lawama zake.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa Tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment