Wednesday, December 16, 2015

RAIS MAGUFULI AIPANGUA TAKUKURU

Rais Magufuli hajaridhishwa mapambano ya rushwa, kaigeukia TAKUKURU

Bado Rais Magufuli anaendelea kuipanga Serikali ya awamu ya tano ili kuhakikisha mambo yanakuwa sawa kwenye utawala wake na kazi inakwenda. Tuhuma za rushwa na ubadhirifu zimekuwa nyingi, baada ya ishu ya makontena bandarini, ukwepaji kodi TRA, kaigeukia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU.
Rais Magufuli amefanya mabadiliko Taasisi ya TAKUKURU na kutengua uteuzi wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Dk. Edward Hoseah ambapo kamteua aliyekuwa Naibu Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Valentino Mlowola kukaimu nafasi hiyo.
Taarifa kutoka Ikulu hii hapa ambapo ametangaza pia kuwasimamisha kazi watumishi wawili ambao walisafiri nje ya nchi kinyume na maagizo yake.
TAKUKURU II
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment