Tuesday, December 22, 2015

POLISI KUIIMARISHA ULINZI KILA KONA KUSHEREHEKEA KRISMASS

Christmas sio kila mtu anasherehekea, hawa hapa watakuwa kazini kama kawaida Uingereza..

December 25 huwa ni siku ambayo wakristo wengi duniani wanaungana kwa pamoja kusherehekea sikukuu ya Christmas, japo sikukuu inawahusu wakristo lakini huwa ni siku ya mapumziko kwa ujumla kwa watu wote bila kujali dini zao.
CHRISTMASS
Sasa nimekutana na hii stori kutoka Uingereza, labda nikufahamishe tu kwamba kama ikitokea December 25 2015 utakuwa na jukumu au ratiba ya kazi usisononeke kwa sababu kuna watu kama 900,000 hivi Uingereza nao watakuwa kazini kama kawaida.
Katika wafanyakazi hao, wapo  168,000 ambao ni watoaji wa huduma za afya na matibabu kama madaktari, manesi pamoja na wauguzi ambao wanatakiwa kuwa kazini kushughulika na majukumu yao ya kila siku.
POLICE
Pia kwenye kundi la wafanyakazi hao, wapo pia Askari Polisi 22,000 pamoja na walinzi 28,000 nao watakuwa kazini pia kuhakikisha usalama wa siku nzima… pia wapo wapishi 42,000 na wahudumu 28,000 wa bar ambao nao watakuwa na kibarua kuhakikisha wanahudumia kwenye maeneo yao ya kazi.
Kwenye idadi hiyo wapo pia watu 20,000 ambao ni watumishi kwenye nyumba za ibada, nao watakuwa kwenye majukumu yao siku hiyo… kwa hiyo kama na wewe uko kwenye majukumu siku hiyo usisononeke, hii ni ripoti kutoka Uingereza pia.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment