Tuesday, December 8, 2015

UCHAGUZI TANGA, ARUSHA

Uchaguzi wa wabunge Tanga na Arusha..

Zikiwa zimebaki siku chache za kupiga kura kwenye uchaguzi wa wabunge Tanga & Arusha..,sasa hapa ninakusogezea kile kilichozungumzwa na Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi Jaji Damian Lubuva kuhusiana na chaguzi hizo.
Taratibu ni zile zile saa kumi jioni ikifika vituo vyote vinafungwa lakini wale ambao wapo kwenye mistari  tutahakikisha kwamba wote watapiga kura….pili mwananchi anapoenda kupiga kura aende na kadi yaani wale waliojiandikisha ili aweze kushiriki zoezi la kupiga kura‘>>>Lubuva
IMG_20151208_073445(1)
Hivyo  kwa mawakala wajibu wao unabaki ule ule kwamba  masilahi ya vyama vyao masilahi ya wagombea wao yanatekelezwa…mawakala wa vyama wa siasa wanaruhusiwa kuwepo vituoni  kwa mujibu wa sheria na kanuni wakala asiyekuwa na barua kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi hatoruhusiwa kuingia katika chumba cha kupigia kura’>>>> Lubuva
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekcuhablog

No comments:

Post a Comment