Monday, December 21, 2015

NAIBU WAZIRI TAMISEMI AWAPIGA MSASA WATUMISHI WA UMMA




Tangakumekuchablog
Tanga, NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais (Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora), Seleman Jaffo, amewataka watumishi wa umma kufanya kazi kwa weledi na kuacha kupikiana majungu na kusema kuwa  yoyote ambaye hawezi kuachia ngazi.
Akizungumza kwenye mkutano mkuu wa pili wa Chama Cha Wafanyakazi Taasisi za Elimu ya juu Tanzania (THTU) juzi mjini hapa, Jaffo alisema ofisi yake haitomvumilia mtumishi ambaye hayuko tayari kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya kazi.
Alisema kuna baadhi ya watumishi wamekuwa chanzo cha kurejesha nyuma maendeleo ya wananchi na kufanya ubadhrifu wa miradi ya maendeleo na hivyo kuagiza yoyote ambaye hayuko tayari kufanya kazi kisheria ni vyema akaachia ngazi.
“Nitoe wito kupitia kwenu najua salamu hizi zitawafikia kwani muko kutoka kila pembe ya taifa letu----mtumishi yoyote wa umma ambaye hayuko tayari kufanya kazi nasi ni bora aachie ngazi” alisema Jaffo na kuongeza
“Serikali imekuwa ikipata malalamiko kila pembe ya ubadhirifu wa pesa za wananchi na utendaji mbovu----hili tunasema halivumiliki na kama ni kutumbua majipu tutasaidiana kuyatumbua” alisema
Aliwataka watumishi haokila mmoja kuwajibika na kuwatumikia wananchi ikiwa lengo ni kuleta maendeleo na kuacha kupikia na majungu ambayo hayana nafasi kwa wananchi na Taifa.
Akizungumza katika mkutano huo, Katibu Mkuu wa THTU, Kulu Maswanya, alimtaka Naibu Waziri, Seleman Jaffo, kulishughulikia tatizo la watumishi kupandishwa vyeo pamoja na malipo.
Alisema kuna tatizo la muda mrefu la  watumishi kupandishwa vyeo na malipo yao kufanyika ya zamani hivyo kumtaka kukifikisha kilio hicho kunakohusika kwa madai kuwa limekuwa sugu.
‘Mheshimiwa Seleman tunakuomba utufikishie kilio chetu cha kupandishwa cheo na malipo-----tumezoea kuona watumishi wakipandishwa vyeo lakini mishaahara yao inabaki vilevile” alisema Maswanya
Aliwataka watumishi hao kufuata maadili ya utumishi wa uma pamoja na kutoa huduma kwa wananchi kwa uadilifu na kuacha kuendesha shughuli kwa njia za panya.
                                                        Mwisho



 Watumishi na Wafanyakazi Taasisi za Elimu za juu Tanzania (THTU) wakiimba wimbo wa mshikamano wa wafanyakazi wakati wa kongamano lilifanyika Tanga juzi.



 Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Thea Ntara, akizungumza na waandishi wa habari wa Tanga mara baada ya kumalizika kongamano la Wafanyakazi Taasisi za Elimu ya juu Tanzania (THTU) lilifanyika juzi.


No comments:

Post a Comment