Saturday, December 19, 2015

RAIS MAGUFULI ATOA MKONO WA POLE WAATHIRIKA WA AJALI BASI

Salamu kutoka kwa Rais Magufuli kwa waathirika wa ajali ya December 18 Iringa..

December 18 2015 nilikusogezea ripoti kutoka Iringa Tanzania, ilihusu ajali ya basi la abiria la Kampuni ya New Force Ltd ambalo lililongana na lori la mbao lilibeba mbao kutoka Njombe kwenda Dar es Salaam… watu 12  walifariki na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli ametuma salamu za rambirambi kwa wote waliofariki kwenye ajali hiyo.
Kwenye barua hiyo toka Ikulu, hii ni nukuu ya alichokisema Rais Magufuli >> ‘Nimesikitishwa sana kutokea ajali hii, ninawapa pole nyingi wote waliopoteza ndugu zao na ninawaombea majeruhi wote wapone haraka ili waungane na familia zao‘- Rais John P. Magufuli.
Barua yote kutoka Ikulu ii hapa
RAIS JPM
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment