Friday, December 25, 2015

WATAKIWA KUWAPENDA WATOTO YATIMA NA WA MITAANI



Tangakumekuchablog
Tanga, WAUMINI wa Dini ya Kikristo wametakiwa kuwa na imni ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu ikiwa na pamoja na kuwapa misaada ya kielimu na kiafya na kuweza kuishi kama wengine.
Akizungumza katika sherehe ya Sikukuu ya Krismass jana, Mchungaji wa Kanisa la Gloryland la Sabasaba, Manase Maganga, aliwataka wazazi na walezi kuwa na moyo wa huruma kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu.
Alisema kuna wimbi kubwa la watoto wanaoishi katika mazingira magumu na kukimbilia mjini ambako hujishughulisha na utumikishwaji wa kazi ngumu na baadhi kujitumbukiza katika vitendo vya uporaji na uvutaji bangi.
“Leo tunasherehekea sikukuu ya krismass wakubwa kwa wadogo pamoja na watoto wetu, furaha hii iwe endelevu kwa wote hata wale wanaoishi katika mazingira magumu” alisema Maganga na kuongeza
“Kuna wimbi kubwa la watoto wa mitaani waliokimbia masomo na wazazi wao na kukimbilia mjini, hili ni janga hivyo kwa pamoja tushirikiane na waweze kupata haki yao ya masomo shuleni” alisema
Maganga alisema watoto wa mitaani wamekuwa kero kwa madai kuwa wengi wao ndio waliojitumbukiza katika vitendo vya uporaji na ubwiaji wa unga na  hivyo kutaka ushirikiano wa wazazi na walezi ili kumaliza tatizo hilo.
Kwa upande wake mzee wa kanisa hilo, Saimon Molely, alisema kanisa hilo kila mwaka limekuwa na da ya kutoa sadaka kwa wazee na watu wanaoishi katika mazingira magumu.
Alisema katika sherehe hiyo wamewasaidia wazee na vijana walioathirika na madawa ya kulevya kwa kuwata Televisheni ili kituoni kwao waweze kujifunza na kujua ubaya wa madawa ya kulevya.
“Tumetoa mashuka nguo na televisheni kwa waathirika wa madawa ya kulevya wanaoishi katika nyumba maalumu , hii ni kuwa siku ya leo ni furaha kwa watu wote” alisema Molely.
Molely alisema kanisa litaendelea kutoa misaada kwa watu mbalimbali wanaoishi katika mazingira magumu wakiwemo wazee na vyakati za majanga hivyo kuwataka waumini wa dini hiyo kuwaombea viongozi wao uzima na afya njema ili kuwatumikia.
                                                    Mwisho



Waumini wa Kanisa la Gloryland Sabasaba Tanga, wakiliombea Taifa amani na kumtakia afya njema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli kutekeleza majukumu yake pamoja na kupiga vita Umasikini na Ufisadi wakati wa Ibada ya Sikukuu ya Krismass jana.



 Kiongozi wa Waathirika wa Madawa ya Kulevya (Soba House) Tanga, Hamza Mkanga, akipokea Televisheni moja, king’amuzi na chupa ya chai kutoka kwa Mchungaji wa Kanisa la Gloryland la Sabasaba Tanga, Manase Maganga, ikiwa ni zawadi ya Krismass

No comments:

Post a Comment