Wednesday, December 16, 2015

LIVE KUTOKA MKWAKWANI

Dk 50, Mwinyi anapiga krosi nzuri ya mpira wa adhabu, Bossou anapiga kichwa juuuuu

Dk 50 Ally Ramadhani anaingia kuchukua nafasi ya Fadhili Kizenga kwa African Sports
Dk 46, Yanga ndiyo wanakuwa wa kwanza kufanya shambulizi, krosi safi ya Msuva lakini Sports wanakuwa imara kuondosha

MAPUMZIKO Dk 45+3 Yanga wanapiga kona, Juma Abdul anapiga ti tak lakini African Sports wanaokoa tena

Dk 44, Ngoma anaruka juu kuuwahi mpira anapiga kichwa lakini dhaibu
Dk 39 hadi 42, mpira unachezwa zaidi katikati ya uwanja na hakuna mashambulizi makali kwa upande wowote ule

SUB Dk 37 Meddy James anakwenda nje kwa African Sports anaingia Mohammed Issa
Dk 33 Kaseke anapiga krosi safi inatua kichwani kwa Kamusoko, lakini kipa anaudaka kwa ufundi kabisa

KADI Dk 31, Pera Mohammed wa African Sports analambwa kadi ya njano kwa kumuangusha Kamusoko

Dk 30, Ngoma anajaribu kupiga shuti kali, lakini linapaa juu ya lango. Bado hakuna mashambulizi makali kwa pande zote

Dk 24 Yanga wanapata kona, inachongwa na Juma Abdul, lakini haina madharaDk 21, Msuva anaingia ndani ya sita ya African Sports lakini anapiga shuti kuuuubwaaaa
Dk 7 hadi 12, mpira zaidi unachezwa katikati ya uwanja, hakuna mashambulizi makubwa na uwanja kuwa na kiwango duni unaonekana kuwa moja ya pingamizi

Dk 6 African Sports wanapata kona baada ya Yondani kuutoa mpira nje. Lakini inakuwa ni kona isiyo na madhara

Dk 5 Msuva anapiga tik tak, lakini kipa anaruka na kudaka vizuri sana
Dk 4 Yanga wanapata mkwaju wa adhabu, Haji Mwinyi anaichonga, unamgonga Msuva na kutoka nje.

Mechi imeanza na Yanga ndiyo wanakuwa wa kwanza kufika katika lango African Sports, lakini linakuwa si shambulizi la kali.

No comments:

Post a Comment