Tuesday, December 29, 2015

MNIGERIA AHUKUMIWA KUNYONGWA MALAYSIA KWA KOSA LA KUKUTWA NA UNGA

Hii ndio hukumu kwa Mnigeria aliyenaswa na ‘unga’ Malaysia..


Kumekuwa na nchi nyingi zikijitahidi kupambana na ishu ya dawa za kulevya Duniani, nchi nyingine imefikia mpaka hatua ya kuweka sheria kali ili kudhibiti kabisa kuingizwa na matumizi ya dawa hizo.
Kwenye list ya nchi ambazo zinatajwa watu wake wengi kukamatwa kwa dawa za kulevya, Nigeria nayo imo !! stori za Wanigeria wengi kutajwa na kukamatwa na dawa za kulevya zimesikika na kugusa pia vichwa vya habari.
Kilichonifikia kutoka Malaysia ni ishu ya Mnigeria mmoja,  Ekene Collins Isaac ambaye amehukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kukutwa na hatia ya kusafirisha dawa za kulevya miaka mitatu iliyopita nchini humo.
Ekene Collins Isaac
Ekene Collins Isaac
Ekene Collins Isaac alikamatwa akiwa amemeza kusafirisha dawa hizo aina ya methamphetamine zenye uzito unaokaribia kilogram moja.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment