Friday, December 4, 2015

KASI YA RAIS MAGUFULI YAANZA KUWAFIKISHA WATUHUMIWA WA MAKONTENA MAHAKAMANI

Watuhumiwa wa kesi ya makontena 349 bandarini walivyofikishwa Mahakamani Dar jana.

Kama ulipitwa na hii stori iliripotiwa kwenye habari ya kituo cha ITV jana  kuhusu ishu ya kufikishwa Mahakamani kwa watuhumiwa kutoka Mamlaka ya TRA ambao walisimamishwa kazi kutokana na kuhusishwa na tuhuma za upotevu wa makontena 349 bandarini Dar.
Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa alipita bandarini siku ya Ijumaa November 27 2015 na kukutana na hiyo ishu ya makontena hayo kupotea na pia kubaini kuwepo kwa ubadhirifu ambao umepelekea Serikali ya Tanzania kukosa mapato kupitia kodi… Jeshi la Polisi likapewa jukumu la kuwakamata watumishi hao 12 na kuendelea na taratibu nyingine za kuwawajibisha.
MAHAKAMANI
Jana  watuhumiwa nane kati wa kesi hiyo wamefikishwa Mahakama ya Kisutu na kusomewa mashtaka ya kesi zao, baadae kesi ikaahirishwa mpaka December 17 2015 ambapo Mahakama hiyo ilikataa kuwapa dhamana watuhumiwa wote.

Hapa ninazo picha kutoka Blog ya Issa Michuzi ilivyokuwa Mahakama ya Kisutu jana.
1
IMG_0879
IMG_0904
IMG_0930
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment