Monday, December 21, 2015

LOIS VAN GAAL KIKAANGONI

Louis van Gaal anaondoka Man United? imenifikia list ya makocha wanaotajwa kuchukua nafasi yake …

Headlines za makocha mbalimbali wa Ligi Kuu Uingereza kufukuzwa zinaendelea kushika kasi ambapo hivi karibuni ulimwengu ulishuhudia Kocha wa Swansea City Garry Monk akifukuzwa na Jose Mourinho akifukuzwa kuifundisha Chelsea.
Stori za mitandaoni za hivi karibuni ni zile zinazomzungumzia Kocha wa Manchester United Louis van Gaal na hatma yake ndani ya klabu hiyo baada ya timu yake kuendelea kufanya vibaya, hivyo kumekuwa na list ya makocha wengine wanaotajwa kurithi nafasi yake mtu wangu.
Kupitia mtandao wa ‘The Telegraph’ pamoja na taarifa zilizopo ndani ya Manchester United zinatajwa, Kocha aliyefukuzwa kuifundisha Chelsea, Jose Mourinho yupo kwenye list ya makocha wanaotajwa kumrithi Van Gaal Man United. Mourinho alifukuzwa na Chelsea baada ya timu hiyo kuwa na mwenendo mbovu.
José-Mourinho
Jose Mourinho
Kocha mwingine anayetajwa ni Pep Guardiola ambaye anaifundisha klabu ya Bayern Munich inayoshiriki Ligi Kuu Ujerumani, kwani hivi karibuni alikataa kuongeza mkataba wa kuendelea kuifundisha  FC Bayern Munich. Mkataba wa Gurdiola ndani ya Bayern unamalizika mwishoni mwa msimu wa 2015/2016.
_78365113_pep_guardiola_getty3
Pep Guardiola
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment