Wednesday, December 16, 2015

MELI MV ROYAL YAWAKA MOTO, ABIRIA WAOKOLEWA

Ripoti kutoka Zanzibar kuhusu ajali ya moto kwenye meli December 15..

Hii stori imenifikia baada ya kuenea kwenye mitandao pamoja na picha zikionesha tukio la meli kuwaka moto
Nimeipata ripoti pia kwenye habari ya ITV kwamba meli hiyo ya MV Royal imepata ajali ya kuwaka moto ikiwa katikati ya safari kutoka Unguja kwenda Pemba, moto huo umeunguza injini za meli hiyo lakini kwa bahati nzuri ikatokea meli nyingine ya MV Serengeti, ambapo ikafanyika kazi ya kuokoa abiria waliokuwa kwenye meli hiyo pamoja na kuuzima moto huo.
MELI
Kamanda wa Polisi Pemba, Shehan Mohamed Shehan amesema meli ilikuwa na abiria zaidi ya 300 pamoja na watoto 70.. wote wametoka salama na meli imefanikiwa kuvutwa mpaka bandarini Pemba.

No comments:

Post a Comment