Sunday, June 12, 2016

WAISLAMU WAASWA KUFANYA WEMA



Tangakumekuchablog
Tanga, IMAMU Mkuu wa Msikiti wa Ibadhi Tanga, Sheikh Mohammed Said, amewataka Waumini wa dini ya Kiislamu wenye uwezo kuwasaidia masikini ili kuweza kutekeleza ibada ya funga kama wenzao.
Akihutubia katika swala ya Ijumaa juzi  ikiwa ni ya mwanzo ndani ya mfungo wa mwezi Mtukufu wa Rmadhani, Mohammed alisema kuna waumini wengi wanafunga lakini hawajui cha kufutaria muda wa jioni.
Alisema mwezi mtukufu wa Ramadhani ni mwezi wa kufanya Ibadan a kutoa ili kuweza kupata rehema na msamaha kwa Mwenyezi Mungu hivyo kuwataka kuisaidia jamii hiyo ili kuweza kuitekeleza Ibada hiyo.
“Ndugu zangu Waislam tuko katika kumi la kwanza la mwezi mtukufu wa ramadhani, ni mwezi wa kheri na machumo kwa mwenye kuzingatia sambamba na mwezi wa toba” alisema Sheikh Mohammed na kuongeza
“Mwezi huu huja mara moja kwa mwaka hivyo inatupasa kuuzingatia na kufanya kila ambalo tunaamini kuwa ni jema na kuweza kuifikia daraja ya mcha Mungu kama wenzetu walivyotutangulia” alisema
Aliwataka watu hao wenye uwezo kuhakikisha waumini wenzao ambao hawana uwezo kuwasaidia kwa hali na mali ili funga yao isiwe ngumu bali kuwa na wepesi na furaha wakati wa kufuturu.
Akizungimzia kuhusu wafanyabiashara kufanya uadilifu na kuuza vyakula kwa bei ya biashara, alisema mwezi huu sio wa kujitafutia utajiri hivyo kuwaasa kuacha kuwalangua wafungaji.
Alisema vipindi vya mwezi wa Ramadhani baadhi ya wafanyabiashara  wamekuwa wakiongeza bei za vyakula ambavyo hutumika kwa futari jambo ambalo ni makosa na huondosha baraka ya biashara.
“Niwakumbushe wafanyabiashara kuacha kupandisha bei za vyakula kwani kufanya hivyo kutawafanya wafungaji kumudu gharama za maisha hasa kuipindi hiki cha mfungo” alisema Mohammed
Aliwataka waumini wa dini hiyo kuwafanyiana  wema pamoja kuhurumiana kwani na kuutaja  mwezi huo  ni wa baraka wenye ujira mkubwa kwa kila jambo ambalo mtu hufanya.
                                              Mwisho

No comments:

Post a Comment