Tuesday, March 31, 2015

ABDUL BONGE AZIKWA KWAO

Kesi ya AT imeisha? Izzo B na show yake Mbeya na mazishi ya Abdul Bonge.

Rock concertIle kesi iliyokuwa imefunguliwa na mganga aliyedai kuwa anamdai msanii AT imemalizika rasmi jana baada ya kukata rufaa, AT amesema kesi hiyo imemalizika rasmi jana baada ya mganga huyo kukata rufaa lakini alikosa ushahidi na baadae iligundulika kuwa hakuwa na sifa za kuwa mganga  kwa kuwa alikuwa hajasajiliwa kufanya kazi za uganga.
izzoWeekend hii msanii Izzo Bizness atafanya show Mkoani Mbeya ambayo imepewa jina la ‘Home Sweet Home Easter Season Concert‘, Izzo amesema show hiyo itafanyika tarehe 05 April, safari hii itakuwa tofauti kwa kuwa anategemea kuambatana na producer Duppy kwa ajili ya kufanya usaili na mtu atakaeshinda atafanyanae kazi, pamoja na surpise nyingi ikiwemo kuonyesha live video ya wimbo wake wa ‘Kidawa’ kwa mara ya kwanza.
MSIBAWAABDULBONGE5Leo wasanii mbalimbali pamoja na wadau wa muziki wamekutana Mkoani Morogoro kwa ajili ya mazishi ya aliyekuwa Mkurugenzi wa kundi la Tip Top Connection, Abdul Bonge aliyefariki Jumamaosi iliyopita, mdogo wake marehemu ambae amesema taratibu za kuupumzisha mwili wa marehemu zinaendelea katika makaburi ya familia huko Mkuyuni.

No comments:

Post a Comment