Monday, March 23, 2015

OSCAR PISTORIUS AGEUKA MWANASOKA GEREZANI

Unaambiwa Oscar Pistorius amegeuka kuwa mwanasoka gerezani?

pistooOscar Pistorius ameendelea kutumikia kifungo chake cha miaka mitano jela baada ya hivi karibuni rufaa yake kukataliwa hivyo kufanya matumaini yake ya kuachiwa kwa dhamana kupotea.
Mwanariadha huyo ambaye ni mlemavu ameonekana akianza kuyazoea maisha ya gerezani ambapo hivi karibuni kuna video ambayo inamuonesha akicheza mpira wa miguu na mwenzake wakiwa ndani ya uwanja wa gereza alilofungwa mjini Pretoria Afrika Kusini.
Gereza la Kgosi Mampuru ambapo mwanariadha huyo amefungwa liliweza kumpunguzia adhabu Oscar huku akipewa uhuru wa kuongea na simu na hata kutembelewa na ndugu zake jambo ambalo limeonyesha kumpa moyo.
Oscar alihukumiwa kifungo cha miaka mitano baada ya kumuua mpenzi wakeReeva Steenkamp kwa kumpiga risasiFebruary 14, 2013 nyumbani kwake.
 https://www.youtube.com/watch?v=faWxQnLhqp4
 Ni halali yako kupata kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment