Wednesday, March 25, 2015

VIMBWANGA VYA WALIMWENGU

Baba wa Yemi Alade alifariki January 16, 2015, sasa wanapanga kufanya mazishi yake!!

restHapa TZ tumezoea kuona mara nyingi ikitokea kuna msiba wa mtu yeyote huwa haichukui muda mrefu kufanya mazishi, labda kuwe na sababu yoyote itakayofanya mazishi yachelewe.. Nigeria iko tofauti, tulianza kuona msiba wa mama yao jamaa wa P Square ambaye alifariki May 11 2012 na kuzikwa August 2 2012, baba yao Moses Okoye alifariki November 24 2014 na kuzikwa January 30 2015.
Huenda ulipata maswali kwamba kwanini mazishi ya wazazi wa mastaa hao yalicheleweshwa?
J.A. Alade ni baba wa msanii Yemi Alade toka Nigeria, mzee huyo alifariki January 16 2015 na taarifa iliyotolewa ni kwamba mazishi ya mzee huyo yatafayika May 7 mwaka huu.
Yemi Alade alisema baada ya kumaliza ziara zake Ulaya atarudi na kuanza maandalizi ya kumzika baba yake lakini hakuweza kueleza ni wapi mazishi hayo yatafanyika.
aladeNitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment