Tuesday, March 31, 2015

MUHAMMADU BUKHARI AIBUKA KIDEDEA NIGERIA

Matokeo rasmi ya Uchaguzi Mkuu Nigeria yanaonesha Wanigeria wameamua hivi..

Muhammadu-Buhari-speech
Siku ya MARCH 28 2015 itakuwa kwenye historia za matukio ya kukumbukwa zaidi Nigeria, walikuwa wakifanya Uchaguzi Mkuu ambapo macho ya wengi Afrika yalikuwa kwenye uchaguzi huo.. Ushindani ulikuwa mkubwa kati ya Rais Goodluck Jonathan ambaye alikuwa madarakani na Muhammadu Buhari.
Kiongozi wa wa chama cha upinzani cha Nigeria ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa Majeshi, Jenerali Muhammadu Buhari amemshinda Goodluck Jonathan kwa zaidi ya kura Mil.2.5.
Goodluck Jonathan alimpigia simu Jenerali Buhari kumpongeza kwa ushindi huo wa kihistoria, ambapo Buhari anakuwa Rais wa kwanza kuongoza nchi hiyo akishinda kutoka Chama cha upinzani.
150120133956_buhari_kano_640x360_ap_nocredit
Nigeria ni moja ya nchi za Afrika ambazo ziliwahi kukumbwa na misukosuko ya Mapinduzi ya Kijeshi, Jonathan amesema katimiza ahadi yake kwamba Uchaguzi huo utakuwa huru na wa haki; “I promised the country free and fair elections. I have kept my word“– Rais Goodluck Jonathan.
Buhari ni mmoja ya wanasiasa ambao waliungwa mkono na mastaa wakubwa wa muziki Nigeria, Tiwa Savage na kundi la Mavins ni sehemu ya waliomsapoti.

No comments:

Post a Comment