Tuesday, March 24, 2015

BREKING NEWS

Taarifa nyingine kubwa ni hii ajali ya ndege iliyotokea Ufaransa…

germanMatukio makubwa ya ajali za ndege ambayo yametokea hivi karibuni na kuingia kwenye headlines ni pamoja na ile ya Malasia Airlines iliyotokea mwaka 2014 ambayo ilipotea na mpaka sasa haijapatikana,na ajali nyingine ni ya Trans Asia ambayo ilipata ajali kutokana na hali mbaya ya hewa na kuua watu wote
Kuna hii nyingine iliyotokea saa chache zilizopita imeripotiwa kuwa ndege ya abiria inayomilikiwa na shirika la ndege la Germanwing Airbus A320 imeanguka katika milima ya Alps nchini Ufaransa.
Ndege hiyo ilikuwa imewabeba abiria 142 na wahudumu 6 wa ndege walikuwa wakitokea katika mji wa Barcelona Uhispania kuelekea Duesseldorf, Ujerumani
Rais wa Ufaransa Francois Hollande amesema kutokana na ajali ya ndege hiyo ambayo mpaka sasa bado inaendelea kuchunguzwa kuna uwezekano mkubwa hakuna mtu yoyote anayeweza kupona.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment