Friday, March 27, 2015

UFISADI KENYA WAMUMIZA KICHWA KENYATA

Ishu ya Ufisadi kwenye Headlines KENYA.. Kingine alichokisema Rais Kenyatta

7A12810D-16F0-4C0B-8DFE-E16EF946A403_mw1024_s_nRais Uhuru Kenyatta jana amehutubia  kikao cha Bunge la taifa hilo kilichofanyika March 26, amewataka maofisa wote wa Serikali waliotajwa katika ripoti iliyotolewa waondoke ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili.
Serikali yangu haina budi kuchukua hatua mahsusi ambayo inalenga kukomesha hili zimwi la ufisadi mara moja, ufisadi umevuka mipaka na lazima nasi tujifunge kibwebwe na kukabiliana nao, natarajia kuwa wale waliotajwa katika ripoti hii watang’atuka mamlakani hadi pale uchunguzi utakapokamilishwa.” Rais Kenyatta.
Ripoti hiyo iliyotayarishwa na tume ya kupambana na ufisadi KACC imetoka wakati ambao kumekuwa na matukio mengi ya ufisadi haswa kwa upande wa Serikali, Mawaziri 5, makatibu 6 na Magavana 10, wametajwa kuwa miongoni mwa maafisa 175 wa umma wanaolazimika kujiuzulu, huku kiongozi wa mashtaka ya umma  ametakiwa kuanzisha uchunguzi ndani ya siku 60.
Katika hotuba hiyo Kenyatta aliwaomba radhi Wakenya waliohujumiwa na Serikali hiyo katika uongozi uliotangulia.
Ili Wakenya waweze kusonga mbele na kusahau yaliyopita kufuatia hatua zilizochukuliwa na Serikali zilizotangulia ni wajibu wangu kuchukua fursa hii na kuwaomba msamaha wote waliodhulumiwa kwa njia moja au nyengine, lazima serikali iombe radhi kwani fedha haziwezi kufuta machungu ya mateso ambayo Wakenya wamepitia’‘–Rais Kenyatta.
Watu 1200 waliuawa katika ghasia hizo huku 650,000 wakiachwa bila makazi kutokana na vita baada ya uchaguzi wa mwaka 2008.
Ni halali yako kupata kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment