Tuesday, March 31, 2015

MTOTO WA MIAKA MIWILI AVUNJA RECORD YA KULENGA SHABAHA

Hii ndio rekodi iliyovunjwa na mtoto wa miaka miwili India

dolly-archer_650x400_81427214935Mara nyingi wazazi hushauriwa kuona umuhimu wa kukuza vipaji vya watoto wao tangu wakiwa wadogo, taarifa ikufikie kuwa mtoto mwenye umri wa miaka miwili ameweka rekodi nchini India kutokana na uwezo wake wa kulenga shabaha ya mishale.
_81884282_81884281Kutokana na vitabu vya kumbukumbu vya rekodi za taifa hilo, mtoto huyo Dolly Shivani Cherukuri, ameweka rekodi ya kuwa mshiriki mwenye umri mdogo zaidi kupata alama 200, katika mashindano yaliyofanyika wiki iliyopita.
288889-2681ba7e-d234-11e4-a4a5-09d7e9cc7466Jarida la Press Trust la India, limesema mtoto huyo alirusha mishale 36 kutoka umbali wa mita 5 na mita 7 na kupata alama 388, tukio lililoshuhudiwa na wachezaji wakongwe na maafisa kutoka idara ya kumbukumbu za michezo.
dolly-archer_650x400_81427214935Baba yake Cherukuri Satyanarayana ambae ni mmiliki wa club moja inayofundisha kurusha mishale amesema, alimfundisha kurusha mishale tangu alipozaliwa, kwa sasa ana mpango wa kumpeleka kushiriki katika mashindano ili afikie hatua ya kuingia kwenye kitabu cha rekodi za dunia cha Guinness.
290181-0a8223fe-d234-11e4-a4a5-09d7e9cc7466


Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment