Saturday, March 28, 2015

YAMEISHA

Baada ya ugomvi wa Madirector wawili wa Tanzania, haya manne ni kutoka kwa Adam Juma.

ad 5Anayo heshima yake kama Director wa video mkongwe kwenye kizazi cha Bongofleva ambae baada ya kuona maneno yakiendelea kurushwa kati ya Madirector wawili kwenye kizazi hikohiko, yani Nisher na Hanscana, Adam ameamua kutoa maneno yake kama kaka.
 katika sanaa za kijinga sana, hazileti maendeleo bali chuki tu, vita kati ya madirector sio jambo la kushangilia hata kidogo, kwani mtu ukiwa wa kwanza wa pili maana yake nini?
‘Mnapoteza urafiki kwa umaarufu wa siku mbili, kitu hiki kilifanyika kwa Pfunk na Mj, then dunga na mapigo then lamar, wako wapi hawa watu ambao ndio mngongo wa mziki, ukiwaangalia hawa maproducer wote ni wakali ila ujinga ndio umesabisha ubishani usiokua na maendeleo’
Kwenye sentensi ya tatu akaandika >>> ‘Tujifunze kupenda na kuangalia style za wenzetu sio kwa lengo la kusema nani ni mkali au nani ni wa kwanza, kwa nia hiyo tutakuza sanaa, sijawahi hata siku moja kufikiria kwamba nimfunike mtu flani au niwe on top, bali nafanya kwa kadri ya uwezo wangu kuwa tofauti, mengine nawaachia watazamaji’
‘Sitaki kufananishwa na mtu yoyote yule kwa uzuri wala ubaya, kama hujaelewa nachokifanya nunua camera fanya wewe, nawaonya nyie mnaogombana mkiwa mmesahau mlipotoka, UMOJA NI NGUVU UTENGANO NI UDHAIFU. Hakuna aliyebora kati yetu wote tunaudhaifu wetu’
ad 1

No comments:

Post a Comment