Tuesday, March 24, 2015

FUMANIZI KATIKA SIMU

Pale ambapo message inafanya afumaniwe na mke wa mtu

Image
Story iliyosikika  leo inahusu ishu iliyotokea maeneo ya Mabibo Hostel ambayo inahusu kijana ambae ni mwanafunzi  wa chuo ambaye kulikuwa na taarifa kwamba ana uhusiano wa kimapenzi na mke wa mtu.
Baada ya kukamatwa na mume wa mwanamke huyo, mwanafunzi huyo amesema kuwa mume wa mwanamke huyo alimkuta akiwa ndani kwake akijaribu kumshawishi mwanamke ili alale nae, lakini anajitetea kwamba ni bahati mbaya tu imetokea hivyo.
Akizungumzia tukio hilo mume wa mke huyo amesema alikuwa amelala akaona message inaingia kwenye simu ya mke wake, alipomuuliza alimwambia hamjui mtu aliyetuma message hiyo.. mwanaume akamwambia amshawishi aje ili amuone.
Kijana huyo alipofika aliingia ndani na kuanza kumbembeleza mwanamke huyo walale, mwanaume akajitokeza na kuanza kumpiga.. mfukoni alikutwa na condom pamoja na shilingi 600.
Baadaye mwanaume huyo alimpeleka Polisi huku akiendelea kujitetea kwamba ni bahati mbaya imetokea hivyo.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment