Friday, March 27, 2015

SIERRA LEONE YAUMIZA KICHWA NA UGONJWA WA EBOLA

Utaratibu huu umerudiwa tena Sierra Leone katika mapambano na Ebola..

makaziSierra Leone ni nchi ambayo imepata athari kubwa zaidi kutokana na ugonjwa wa Ebola tangu ugonjwa huo ulipoanza zaidi ya mwaka mmoja sasa, athari yake sio kwa watu waliofariki ama kupata maambukizi ya Ebola pekeyake, imefikia hatua hata ya uchumi wa nchi hiyo kuwa kwenye hali mbaya, shule zimefungwa na vitu vingine vingi kusimama.
Hii sio mara ya kwanza Serikali kutoa agizo kama hili ambalo limetolewa la watu wote kukaa ndani kwa siku tatu kuanzia leo March 27 mpaka Jumapili March 29 ili wafanye ukaguzi wa nyumba hadi nyumba kujua kama kuna watu ambao wana dalili za ugonjwa huo waweze kuwapata na kusaidia watu wengine wasipate maambukizi hayo.
.
Hawa ni baadhi ya watu ambao wanafanya ukaguzi kwenye nyumba kama kuna watu wenye dalili za ugonjwa huo.
.
Hali ilivyo mitaani baada ya agizo lililotolewa na Serikali kuzuia watu wasitoke nje kwa siku tatu.
Siku ya Ijumaa zimetolewa saa mbili tu kwa waislamu kwenda kuswali, siku ya Jumapili pia zitatolewa saa tano kwa ajili wakristo kwenda kusali.
.
Mitaani kuna vizuizi kabisa ambavyo vimewekwa na askari wapo kuhakikisha hakuna watu wanazunguka.
Mataifa matatu ya Afrika Magharibi yalioathiriwa vibaya na Ebola ni Sierra Leone, Liberia pamoja na Guinea na zimepanga kuhakikisha zinatokomeza ugonjwa huo ifikapo.
.
Serikali na taasisi mbalimbali zimetoa msaada wa chakula kwa watu wenye mahitaji.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment