Monday, March 23, 2015

ATAKA KUMTOA UHAI MAMA YAKE , KISA KUPOKWA SIMU YA IPAD

Maamuzi ya binti huyu kwa mama yake nayo kwenye headlines!!

poisonMatukio ya wazazi kuwa na ugomvi na watoto wao wa kuwazaaa wenyewe huwa ni jambo la kawaida kutokea ndani ya familia lakini inapofikia hatua ya watu hao kutaka kutoana uhai kwa lengo la kulipiza kisasi huleta picha nyingine kabisa kwenye jamii.
Hii imetokea huko Marekani baada ya mama mmoja kunusurika kifo mara mbili baada ya mtoto wake kumwekea sumu ya kuondoa madoa kwenye kinywaji chake kisa kikiwa ni baada ya kumnyang’anya simu yake aina ya Iphone.
Mtoto huyu mwenye miaka 12 katika jimbo la Colorado Marekani amefunguliwa mashtaka ya kuua na amekiri kuwa alitaka kumuua mama yake ili kulipiza kisasi kwa sababu alichukua simu yake.
Mara ya kwanza mtoto huyo alimwekea mama yake sumu aina ya Chlorine kwenye kinywaji na mama yake hakuweza kubaini ingawa alisema alisikia harufu lakini alihisi glasi aliyotumia haikuoshwa vizuri.
Mama yake aliwaambia maafisa wa polisi kuwa alishangaa aliponusa harufu ya sabuni baada ya kunywa mchanganyiko huo uliotayarishwa na mwanaye huyo.
Ni halali yako kupata kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment