Sunday, March 29, 2015

CHANZO CHA KIFO CHA ABDUL BONGE HIKI HAPA

Tulizipokea taarifa za kifo cha Abdul Bonge wa Tiptop Connection ila hiki ndio chanzo cha kifo

RIPSaa zinahesabika toka Tanzania na familia ya bongofleva ipokee taarifa za msiba wa Abdul Bonge Mwanzilishi wa kundi maarufu la Bongofleva Tiptop Connection lenye wanachama kama Tunda Man, Madee, Dogo Janja na wengine waliopita kama Keisha, Cassim Mnganga na MB Dogg.
Jioni ya March 28 2015 ndio taarifa zilianza kusambaa katika mitandao  lakini chanzo cha kifo cha ghafla cha Abdul hakikuwa kimesemwa lakini mdogo wake ambae ni Babu Tale amewka bayana. na kusema >>> ‘Kuna mshkaji wetu mmoja alikua anagombana na mke wake jirani yetu, wakamfata hapa Abdul aende… mara ya kwanza na ya pili akakataa, mara ya tatu akasema ngoja aende’
Abdu Bonge na Bab TaleAlivyoenda ukapita ukimya kidogo, baadae kuna mtu akaja kumuita kaka yetu mkubwa mwingine na kumwambia nenda kamsaidie kaka yako mkubwa amedondoka, kaka yangu baadae akanipigia simu akasema Bonge kama amezimia lakini sidhani kama atapona sababu wakati wa kuamulia ugomvi alianguka baada ya kusukumwa nafikiria aliangukia kichogo, kumpeleka Hospitali Manzese wakasema ameshafariki‘ – Babu Tale.
Hutopitwa na habari inayonifikia na niko tayari kukutumia muda wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment