Thursday, March 26, 2015

NI VILIO TU, AJALI YA NDEGE YA GERMANWINGS

Ajali ya ndege:rubani alifungiwa nje

Ndege ya Germanwings ilipokuwa ikisafiri katika anga la Duesseldorf nchini Germany mwaka 2014.

Mkurugenzi wa shirika la ndege la Germanwings, Thomas Winkelmann amesema wasafiri 72 kati ya 144 walikuwa raia wa Ujerumani.
wengine walikuwa ni kutoka nchi za Australia, Argentina, Iran, Venezuela, Marekani, Uholanzi, Colombia, Mexico, Japan, Denmark na Israel.
Ramani ikionesha eneo la ajali ya ndege ya Ujerumani
Uchunguzi wa awali wa sauti zilizokuwa ndani ya kifaa cha kurekodia sauti ya ndege iliyoanguka Ufaransa unaonesha kuwa moja wa marubani wa ndege hiyo alikuwa amefungiwa nje ya eneo la marubani wakati ndege hiyo ilipoanguka.

Milima ya Alps, eneo ambalo ajali ya ndege ilitokea.

.
Wanafunzi katika shule ya Haltern-am-See nchini Ujerumani wakilia baada ya wenzao kupata ajali kwenye ndege ya Germanwing.

Waokoaji wakijadiliana katika eneo la ajali mapema leo asubuhi

No comments:

Post a Comment