Tuesday, March 31, 2015

ANA MIAKA 56 WATOTO 40

Mzee na watoto wake 40… kingine anachokiwaza ni hiki!!

babaUzazi wa mpango ni jambo ambalo husisitizwa mara nyingi  ili kuwa na familia bora na uwezo wa kutunza familia kutokana na idadi ya watoto wanaozaliwa.
Mike Holpin hakuona umuhimu wa ishu ya uzazi wa mpango,  mpaka sasa ana watoto 40 na bado anafikiria kuongeza wengine huku akiamini hata vitabu vya dini vinaruhusu hilo.
Mwanaume huyo mwenye miaka 56 mwenyeji wa Monmuothshire, Uingereza alipata mtoto wake wa kwanza akiwa na miaka 19 tu na kwa sasa mtoto wake wa kwanza ana miaka 37 huku wa mwisho akiwa na miaka mitatu.
mgongoWatoto hao amezaa na wanawake 20 tofauti na amesisitiza kuwa yupo tayari kuongeza wengine kwani hata vitabu vya dini vimeruhusu na ameamua kujichora tattoo zenye majina ya watoto wake mgongoni ili aweze kuwakumbuka.
Aliongeza kati ya wanawake 20 aliowazalisha sita ndio aliweza kuishi nao lakini baadae alitengana nao kutokana na tabia yake ya kutokuwa mwaminifu pamoja na kuwanyanyasa.
Hakuna Stori itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment