Tuesday, March 17, 2015

AFUNGWA MIAKA 7 JELA KWA KOSA LA KUMTOA UJAUZITO MWENZA WAKE

Hiki alichokifanya kuutoa ujauzito wa mpenzi wake ni ishu ambayo imechukua headlines !

woman-holding-cocktail-glass-barMwanaume mmoja Norway anashikiliwa kwa tuhuma za kumsababishia majeraha mpenzi wake pamoja na kumtoa ujauzito bila ridhaa yake, baada ya kumuwekea vidonge kwenye kinywaji na kusababisha ujauzito wake kuharibika.
Jamaa huyo alifanya ukatili huo baada ya kumuwekea mpenzi wake vidonge ya kutoa mimba kwenye kinywaji alichokuwa anakunywa kwa lengo la kumtoa ujauzito wa miezi minne aliokuwa nao, ambapo alifikia hatua hiyo baada ya kumshawishi kuutoa kwa muda mrefu bila mafanikio.
Mwanamke huyo amesema mpenzi wake alikuwa akimshawishi mara nyingi kutoa ujauzito huo lakini hakukubaliana nae, baada ya kunywa kinyaji hicho alisikia maumivu makali ya tumbo na ujauzito wake kutoka, alipoenda Hospitali na kufanya vipimo ilionekana ujauzito wake umeharibika tayari.
Hata hivyo mtuhumiwa huyo alikiri kufanya kosa hilo na kusema anajisikia vibaya ila amefanya hivyo kwa sababu ilikuwa njia pekee ya kufanikisha lengo lake kuutoa ujauzito huo, Mahakama imemhukumu kifungo cha miaka saba jela.
Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia  www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment