Monday, March 16, 2015

VIMBWANGA VYA WALIMWENGU

Baba kaamua kumchoma mtoto wa jirani yake kulipiza kisasi

400103781475Tukio lililojiri leo ishu ya baba mmoja kumuunguza mtoto  wa jirani kama njia ya kuulipiza kisasi cha mtoto wake kuunguzwa kwa bahati mbaya wakati wakicheza na wenzake.
Mtoto huyo amesema alikuwa anatoka nje akiwa amebeba sufuria la moto, mtoto mmoja akatokea akiwa anakimbia na kugongana naye, mtoto huyo akaumia kwa bahati mbaya kichwani.
Baadae watoto waliokuwa uwanjani wanacheza, baba wa mtoto aliyeunguzwa alimuita mtoto ambaye alimumiza mwanae na kwenda naye nyumbani kwake, akaweka kisu jikoni na kumchoma nacho sehemu mbalimbali mwilini kama kulipiza kisasi.
Majirani baada ya kugundua tukio hilo waliamua kwenda kushtaki Serikali za mitaa kutokana na mama ambaye mtoto wake amechomwa kulipiza kisasi kuogopa kutoa taarifa akihofia kufukuzwa kwenye nyumba hiyo aliyopangishwa na baba ambaye kamchoma mwanae.
Polisi walifika eneo hilo na kumkamata mtuhumiwa.
Ni halali yako kupata kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment