WAHAMIAJI HARAMU 64 RAIA WA ETHIOPIA WAKAMATWA MKOANI DODOMA
Jeshi
la Polisi Mkoa wa Dodoma kwa kushirikiana na Wananchi imewakamata
Wahamiaji haramu 64 raia wa nchi ya ETHIOPIA (Wahabeshi) katika Kijiji
cha KIDOKA, Kata ya KIDOKA, Tarafa ya GOIMA, Wilaya ya na CHEMBA Mkoa
wa DODOMA, mmoja kati yao alikutwa akiwa amefariki aliyetambuliwa
kwa jina moja la TAJIRU anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 –
30. Watu hao walikuwa wakisafirishwa kwa Lori aina ya Mitsubishi Fuso lililokuwa likiendeshwa na OTHMAN YUNUS
MTEKATEKA, miaka 45, na Mkazi wa ILALA Jangwani jijini Dar es Salaam
akitokea Moshi - Kilimanjaro kwenda mkoani Mbeya.
Sehemu ya Wahamiaji haramu 64 raia wa nchi ya ETHIOPIA (Wahabeshi) wakiwa hoi na kupatia huduma za kiutu zikiwemo chakula na matibabu.
|
No comments:
Post a Comment